HABARI

Italy imeathirika zaidi na Corona kuliko China

Italy imeathirika zaidi na Corona na inaripotiwa kuwa hadi kufikia usiku wa Alhamis Machi 19, 2020 idadi ya vifo vitokanavyo na Covid19 ilifikia 3,405 ambapo vifo vipya 427 vilitokea kwa siku hiyo.
Aidha, idadi hiyo ya vifo nchini Italia inaipiku ile ya China ambapo vifo vilivyotokea ni 3,245 tangu iliporipotiwa kwa muathirika wa kwanza mwishoni mwa mwaka 2019.
Mpaka sasa taifa la Italia ndilo lililoathirika zaidi na Corona virus ukilinganisha na China ambako ndiko virusi hivyo vilianzia.

About the author

kidevu

Leave a Comment