HABARI

Mbinu Mpya za Wanawake wa Siku Hizi Wanaosaka Ndoa Kwa Nguvu..Ni Noma Sana

Siku ya kwanza atakuja na chupi 2, moja anaifua anaacha bafuni,nyingine anavaa asubuhi anaondoka…
Siku ya 2 anakuja na khanga,anaivaa usiku,asubuhi anaianika nyuma ya mlango anaondoka…

Siku ya 3 anasahau pete na hereni juu ya meza anakwambia ‘Hny nitunzie nimesahau hereni zangu mezani

Siku ya 4 anakuja na nguo 2 na vipedo vya kubadilisha na viatu pea 2,anavua high heels anaweka kwenye Shoe rack,asubuhi anaondoka na flat shoes kwenda chuo. Baada ya mwezi chumba chako kinakuwa na vitu kadha wa kadha,na ole wako uvihamishe alipoacha,kesi zinaanza…

Hao ndo Wanawake wa kileo,akija na begi zima si utamuuliza Vipi mwenzangu na utamkimbiza…Anahamia taratibu.. Mwisho wa siku dressing table yako iliyokuwa ina perfume na mafuta ya Rays inakuwa imejaa hereni na ‘Foundation’…

My Brother,huna haja ya kuuliza,NDO KASHAHAMIA HUYO….
Kifuatacho utaambiwa,”Honey I miss my days’,Zamani nilijua ni Simu za mkononi tu ndo zina Missed Calls, Siku hizi kuna Missed days,ukiambiwa hivi tu jua imekula kwako, inawindwa ndoa hapo…

About the author

kidevu

Leave a Comment