HABARI

Pigo la uncle na mama watoto, Mayweather ashindwa kurejea Ulingoni 2020

Bondia wa Marekani Floyd Mayweather imeripotiwa kuwa amefuta mpango wale wa kurudi ulingoni kupigana mwaka 2020 kutokana na kupata misiba miwili mizito ndani ya wiki moja.
Floyd ikiwa sio zaidi ya wiki moja alipoteza watu wawili muhimu, March 9 alimpoteza mpenzi wake wa zamani na mama watoto wake watatu Josie Harris na March 17 alimpoteza baba yake mdogo na kocha wake Roger Mayweather kwa kisukari.
Hivyo ripoti zinadai hana mpango wa kurudi ulingoni kutokana na hayupo fiti kisaikolojia, Floyd Mayweather alikuwa akihusishwa kurudi ulingoni 2020 ili arudiane na Conor McGregor na Manny Pacquiao.

About the author

kidevu

Leave a Comment